JUMAPILI KUU YA MWILI NA DAMU YA YESU KRISTO-11/06/2023

MATANGAZO:  JUMAPILI KUU YA MWILI NA DAMU YA YESU KRISTO – 11/06/ 2023

  1. Leo ni Jumapili ya fungu la kumi,kwa wakristo ambao wamejitayarisha na pia wale ambao wametuma fungu lao la kumi  kwa paybill ya kanisa  tunawaalika wajongee mbele kwa maombi na baraka.Tunapokuja mbele tunaombwa kuweka nia zetu pamoja na fungu la kumi tunalomtolea Mungu.Paybill ya kanisa ni 4042525 account Tithe.
  2. Leo, Kanisa linasherehekea Siku Kuu ya Mwili na Damu ya Kristo (Corpus Christi). Punde tu baada ya Misa hii, kutakuwa na ibada ya kumwabudu Bwana wetu Yesu Kristu, aliye hai katika Sakramenti Takatifu ya Ekaristi.
  3. Wakristo ambao waliacha kupokea  na hawako kwa ndoa na wangependa kurudi kupokea Sakramenti Takatifu, wanaombwa kuona Padre kwa ofisi siku na masaa ya kazi au, wapige simu kujadiliana na Padre siku ingine yeyote wanaweza kupatikana.
  4. Josil Ushindi group watakuwa na siku ya maombi Jumamosi ijayo tarehe 17/06/2023 kuanzia saa tatu asubuhi.
  5. Kikundi cha kina Baba (CMA) wanaalikwa kwa mafundisho yao Jumapili ijaya ya tarehe 18th June 2023 baada ya Misa ya kwanza
  6. Padre kutoka Lodwar atatembelea Parokia yetu Jumapili ijayo tarehe 18th Juni 2023. Kupongeza Wakristo kwa ukarimu ambao tumeonyesha   familia ya Lodwar na pia kuomba msaada ili aweze kuendelea kuhudumia wakristo wa Lodwar.  Wakristo wanakaribishwa kuchukua bahasha ambazo tutamkabidhi mgeni wetu Jumapili ijayo.
  7. Tumeanza usajili wa Watoto wachanga kwa ajili ya ubatizo. Wazazi wanaopenda Watoto wao wachanga wabatizwe wanaombwa kujiandikisha katika Jumuiya zao.

          Jumuiya service

            Jumapili Hii                                                               Jumapili Ijayo

1st Mass: St. Rita                                                      1st Mass: St. Gabriel

2nd Mass: St. Timothy                                              2nd Mass: CWA

 

Matangazo ya Siku Kuu ya Pentekoste,28/05/2023.

MATANGAZO – PENTECOST SUNDAY 28/5/2023

1.Wakristo ambao waliacha kupokea  na hawako kwa ndoa na wangetaka kuanza kupokea Sakramenti Takatifu, wanaombwa kuona Padre kwa ofisi siku na masaa ya kazi au, wapinge simu kujadiliana na Padre siku ingine yeyote wanaweza kupatikana.

2.Jumamosi ijayo (3/6/2023) ikiwa ni Jumamosi ya kwanza ya mwezi, ni siku ya maombi(recollection) kuanzia saa tatu asubuhi (9.00am) hadi saa sita mchana (12:00 noon). Hakutakuwa Misa ya asubuhi kama ilivyo kawaida.

3.Alhamisi tarehe moja June (1st June) ambayo Wakenya watasherehekea  Madaraka day, Misa itaanza saa tatu asubuhi (09.00am).

4.Jumapili ijayo tarehe nne June (4th June) vijana kutoka Ngong Cathedral Plan watatembelea kanisa yetu ili wawe na kikao maalum pamoja na vijana wetu. Vijana wote wanahimizwa kuhudhuria siku hiyo.

5.Kikundi cha Josil Ushindi (Singles Church Support) wanakubushwa mkutano wao baada ya hii Misa. Wakristo ambao ni single na wangetaka kujiunga na kikundi hiki wamekaribishwa.

6.Jumapili ijayo tarehe 4/6/2023 wahudumu kutoka hospitali ya Equity Afia, watatembelea kanisa letu kupeana vipimo tofauti tofauti kwa bei nafuu. Wakristo wanaombwa kuchukua fursa hii kujua hali ya afya yao.

7.Jumuiya service

1st Mass: St. Joseph the Worker                              1st Mass: St. Raphael

2nd Mass: St. Padre Pio                                               2nd Mass: Senior Youth

 

8. Matangazo ya PFC